HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, February 6, 2018

STARTIMES YAMKUTANISHA STAA MAU DOU DOU NA WASANII WA FILAMU NCHINI

Kampuni ya Star Media (T) Ltd kupitia chapa yake ya StarTimes imefanya hafla fupi ya kumkutanisha muigizaji maarufu wa China Hai Qing maarufu kama Mau Dou Dou na wasanii wa Kitanzania pamoja na mashabiki wake.

Hafla hiyo ilifanyika katika ukumbi wa kimataifa wa Mikutano wa Mwalimu Nyerere (NICC) na kuhudhuriwa na wasanii mbalimbali maarufu akiwemo Natasha, Yvone na Davina. 

Mwigizaji maarufu wa China, Hai Qing maarufu kama Mau Dou Dou amekuja nchini Tanzania kwa ziara ya siku mbili ambapo moja ni kutangaza kampuni ya Startimes.

Makamu wa Rais wa Startimes Tanzania, Zuhura Hanif amesema kuwa msanii huyo sehemu kubwa anatangaza Kiswahili katika king’amuzi cha Startimes.

Amesema kuwa msanii huyo amekuwa na kazi nyingi kwa Ubalozi wa nchini China pamoja na Startimes ikiwa ni kukuza Kiswahili.
Mwigizaji maarufu wa China, Hai Qing "Mau Dou Dou" (kushoto) akizungumza jambo kwenye mkutano na waandishi wa habari, wasanii wa filamu nchini pamoja na mashabiki wake leo Jijini Dar es Salaam
Meneja Masoko na Mahusiano wa StarTimes Tanzania, Juma Sharobaro(kulia) akifanya mahojiano na Mwigizaji maarufu wa China, Hai Qing "Mau Dou Dou"  alipokutana na wasanii wa filamu pamoja na mashabiki wake leo kwenye ukumbi wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam. 
Makamu wa Rais wa Startimes Tanzania, Zuhura Hanif (kulia) akimkabidhi tuzo Mwigizaji maarufu wa China, Hai Qing "Mau Dou Dou" (kushoto)  kwa niaba ya watanzania ambao ni mashabiki wake
Msanii wa filamu nchini Tanzania, Suzan Lewis "Natasha "(kulia) akitoa shukrani kwa niaba ya wasanii wa filamu nchini wakati wa ziara ya  Mwigizaji maarufu wa China, Hai Qing "Mau Dou Dou"  alipofika na kufanya mazungumzo nao leo jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya wasanii wa Filamu nchini pamoja na mashabiki wa Mwigizaji maarufu wa China, Hai Qing "Mau Dou Dou"  wakifuatilia mada wakati wa mkutano huo.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad