HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, December 21, 2017

YALIYOJIRI KATIKA ZIARA YA KAMISHNA WA UHAMIAJI ZANZIBAR, MKOA WA KASKAZINI PEMBA

Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Pemba, Bwana Omari Khamis Othman Akizungumza na Kamishna wa Uhamiaji Zanzibar, Johari M. Sururu (kulia) na Ujumbe aliofuatana nao alipomtembelea ofisini kwake, wakati akiendelea na ziara ya kikazi Mkoani humo tarehe 20 – 21 Disemba, 2017. Mkuu huyo wa Mkoa aliahidi kushughulikia kwa karibu ombi lilitolewa na Kamishna Sururu, la kupatiwa Viwanja kwenye maeneo yaaliyotengwa na Serikali ili kujenga Nyumba za Makaazi ya Askari wa Jeshi la Uhamiaji Mkoani humo. 
 Kamishna wa Uhamiaji Zanzibar, Johari M. Sururu akisikiliza maelezo yanayotolewa na Mkaguzi Msaidizi wa Uhamiaji, Iddi A. Iddi wa Kituo cha Uhamiaji Bandari ya Wete, kuhusu ukaguzi wa Watu wanaotumia Bandari hiyo, ambapo vyombo vyake havijaruhusiwa kisheria kusafirisha abiria. Ilielezwa kuwa hiyo ni changamoto kubwa katika Bandari hiyo kwani abiria wengi wanaotumia Bandari hiyo hudai kuwa wanakwenda kwenye visiwa vya jirani vya Fundo, Uvinje na Kokota, badala yake wakifika Bandari bubu zilizoko kijiji cha Mtambwe wanabadili chombo kuelekea Visiwa vya Mombasa, Kenya. Yalisemwa hayo wakati wa ziara ya kikazi Mkoa wa Kaskazini Pemba tarehe 20 – 21 Disemba, 2017. 
 Mkuu wa Bandari ya Wete, Bwana Hassan Hamad Ali akimpokea na kumkaguza maeneo mbali mbali ya Bandari hiyo Kamishna wa Uhamiaji Zanzibar, Johari M. Sururu (wa pili kushoto) na Maafisa Waandamizi wa Uhamiaji aliombatana nao katika ziara ya kikazi Mkoa wa Kaskazini Pemba tarehe 20 – 21 Disemba, 2017. Kamishna Sururu alimtaka Mkuu huyo kushughulikia kwa karibu changamoto iliyopo ya baadhi ya vyombo vya Usafiri “Majahazi” bandarini hapo kupakia abiria kinyume cha Sheria.  
 Mkaguzi wa Uhamiaji, Omari Saidi Mohamed akimuonesha Kamishna wa Uhamiaji Zanzibar, Johari M. Sururu (katikati) na Maafisa Waandamizi wa Uhamiaji Aliombatana nao Nyumba za Makaazi ya Askari wa Uhamiaji zilizoko mtaa wa Mtemani, Wilaya ya Wete, Mkoa wa Kaskazini Pemba wakati wa ziara ya kikazi Mkoani humo tarehe 20 - 21 Disemba, 2017. Kutokana na uchakavu wa nyumba hizo, Kamishna Sururu aliagiza nyumba hizo zifanyiwe ukarabati haraka iwezekanavyo, huku akiahidi kwamba, Idara yake kwa kushirikiana na Serikali 
 Sheha wa Shehia ya Gando, Bw. Jafari Suleiman Said (wa pili kulia) akizungumzia uwepo wa Bandari bubu ya Chokaani, Shehia ya Gando Wilaya ya Wete inayotumiwa na baadhi ya watu kuingia na kutoka Visiwani humo kwenda visiwa vya Mombasa, Kenya. Hayo yalielezwa kwa Kamishna wa Uhamiaji Zanzibar, Johari M. Sururu wakati akiendelea na ziara yake ya kikazi Mkoa wa Kaskazini Pemba tarehe 20 – 21 Disemba, 2017. 
 Kamishna wa Uhamiaji Zanzibar, Johari M. Sururu (wa pili kulia) akiwa mbele ya Jengo la Ofisi ya Uhamiaji Wilaya ya Micheweni, Mkoa wa Kaskazini Pemba iliyofanyiwa ukarabati mkubwa na kujengwa uzio hivi karibuni, akifafanua jambo kuhusu mkakati wa Idara wa kuboresha Majengo ya Ofisi na Makaazi ya Askari wa Uhamiaji kwa Mikoa yote Unguja na Pemba. Huo ni muendelezo wa ziara ya kikazi Mkoani humo tarehe 20 – 21 Disemba, 2018. 
 Kamishna wa Uhamiaji Zanzibar, Johari M. Sururu (wa pili kushoto) akipokea salamu za Wananchi wa Shumba Mjini, akiwa katika ziara ya kikazi tarehe 20 Disemba 2017, akitembelea Bandari Bubu iliyopo Shumba Mjini, Wilaya ya Micheweni, Mkoa wa Kaskazini Pemba, ambayo ni maarufu kwa shughuli za Uvuvi na Biashara.  
Mkuu wa Diko “Bandari Bubu” ya Shumba mjini Bwana Hussein Rashid Omar, akimuonesha Kamishna wa Uhamiaji Zanzibar Johari M. Sururu wakati alipofanya ziara ya kikazi Wilaya ya Micheweni, Mkoa wa Kaskazini Pemba tarehe 20 Disemba, 2017, baadhi ya Majahazi (hayapo pichani) yanayofanya safari zake kupitia Bandari bubu hiyo. Huku wananchi waliowazunguka wakisisitiza kuwa wao wanuafata Sheria na Taratibu zote za Nchi wanapotoka ama kuingia nchini ikiwemo matumizi ya Pasipoti na kuiomba Idara ya Uhamiaji kusukuma mbele juhudi za Serikali kurasimisha Bandari hiyo 
 Sheha wa Shehia ya Kiuyu Mbuyuni, Bw. Ali Hamad Sharifu (wa pili kulia) akimueleza Kamishna wa Uhamiaji Zanzibar, Johari M. Sururu (kushoto kwake), jinsi wanavyoshirikiana na watendaji wa Idara ya Uhamiaji kwa kutoa taarifa zinazosaidia kuwadhibiti baadhi ya Watu wasio waaminifu wanaojaribu kuingiza wageni bila ya kufuata Sheria na Taratibu za Idara ya Uhamiaji Nchini. Yalielezwa hayo wakati Kamishna akiendelea na ziara ya kikazi, Mkoa wa Kaskazini Pemba tarehe 20 – 21 Disemba, 2017. 
Kamishna wa Uhamiaji Zanzibar, Johari M. Sururu akiambatana na Maofisa waandamizi wa Idara ya Uhamiaji Zanzibar kukagua baadhi ya bandari Bubu za Kiuyu na Mbuyuni, Wilaya ya Micheweni, Mkoa wa Kaskazini Pemba wakati alipofanya ziara ya kikazi maeneo mbali mbali, Mkoani humo tarehe 20 – 21 Disemba, 2017. Wilaya ya Micheweni ina Bandari Bubu zaidi ya 80 Zinazotumiwa kuvuka mpaka wa majini kuingia Visiwa vya jirani pamoja na Shimoni, Mombasa, Kenya ambapo wakaazi wa maeneo hayo wana muingiliano mkubwa katika shughuli za kiuchumi na kijamii. 

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad