HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, December 21, 2017

NAIBU WAZIRI SHONZA AFUNGA MICHEZO YA VYUO VIKUU TANZANIA (TUSA) MJINI DODOMA

 Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Juliana Shonza akizungumza na washiriki wa Michizo ya Vyuo Vikuu (Hawapo Pichani) wakati akifunga fainali za Michezo hiyo iliyofanyika Chuo Kikuu cha Dodoma mjini Dododma leo Tarehe 20/12/2017. Waliokaa kulia kwake wa kwanza ni Naibu Waziri wa Kazi, Ajira na Vijana Mhe. Antony Mavunde,Wa pili ni Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dodoma Prof. Idris Kikula na Mtangazaji wa Clouds Fm Ndg. Shafii Dauda.  
Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Juliana Shonza akijiandaa kufunga kikapu wakati wakufunga Michezo ya Vyuo Vikuu kwenye Mchezo wa Fainali ya mpira wa kikapu kati ya timu ya Chuo Kikuu Kishiriki cha Tanzania (OUT) na Chuo Kikuu cha Dododma (UDOM) iliyofanyika Chuo Kikuu cha Dodoma mjini Dododma leo Tarehe 20/12/2017, wa Pili kushoto ni Naibu Waziri wa Kazi, Ajira na Vijana Mhe. Antony Mavunde. OUT waliibuka washindi wa mchezo wa kikapu kwa wanaume.
 Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Juliana Shonza akimvisha medali golikipa wa timu ya mpira wa miguu ya Chuo Kikuu cha Zanzibar Ahmad Suleiman wakati wa kufunga fainali za Michezo ya Vyuo Vikuu iliyofanyika Chuo Kikuu cha Dodoma mjini Dododma leo Tarehe 20/12/2017. Chuo Kikuu cha Zanzibar waliibuka washindi wa mpira wa  miguu kwa wanaume.
 Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Juliana Shonza akisalimiana na wachezaji wa timu ya mpira wa kikapu ya Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT) wakati wa kufunga fainali za Michezo ya Vyuo Vikuu iliyofanyika Chuo Kikuu cha Dodoma mjini Dododma leo Tarehe 20/12/2017. OUT waliibuka washindi wa mchezo wa kikapu kwa wanaume dhidi ya Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM)

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad