HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, December 28, 2017

JESHI LA POLISI MKOANI NJOMBE LINAMSAKA ASKARI PC ZAKAYO DOTO KWA TUHUMA ZA MAUAJI

Kamanda wa polisi Mkoa wa Njombe,  Pudensiana Protasi akizungumza na waandishi wa habari 

Na Amiri Kilagalila, Njombe
Jeshi la polisi  mkoani Njombe linamtafuta askari PC Zakayo Doto kwa kosa la kumuua kwa kumpiga risasi askali wa jeshi la wananchi (JWTZ) anayedaiwa kuwa ni mchumba wake kwa kile kinachodaiwa ni wivu wa mapenzi.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa majirani wa mtaa wa Jeshini kata ya Makuvani wanasema marehemu Neema Masanja aliyekuwa askari wa Jeshi la Wananchi kikosi cha 514KJ Makambako alipigwa risasi na askari PC Zakayo Doto ambaye anadaiwa kuwa ni mchumba wa marehemu huku sababu zikiwa bado hazijafahamika

Mganga mfawidhi wa hospitali ya mji wa Makambako daktari Kesha Ngunda amekiri kupokea mwili wa marehemu afande Neema Masanja ambao umefikishwa hospitalini hapo kwa ajili ya uchunguzi.

Kamanda wa polisi mkoa wa Njombe Pudensiana Protasi amethibitisha kutokea kwa tukio hilo.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad