HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, December 28, 2017

BENKI YA CRDB YAANZA MCHAKATO WA KUPATA MRITHI WA DKT. KIMEI

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dkt. Charles Kimei (katikati) akizungumza na waandishi wa Habari ofisini kwake jijini Dar es salaam leo, kuhusu Benki hiyo kuanza mchakato wa kumtafuta mrithi wa nafasi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, unaotaraji kuanza mapema mwakani. Huku akiwatoa hofu wateja na wananchi kiujumla kuwa Benki ipo salama. Dkt. Kimei atandelea kuhodhi nafasi hiyo mpaka Mei 2019 atakapostaafu. Kulia ni Mkurugenzi wa Masoko, Utafiti na Huduma kwa Wateja wa Benki ya CRDB, Tully Ester Mwambapa na kushoto ni Mkurugenzi wa Mikopo wa Benki ya CRDB, James Mabula.
Mkurugenzi wa Masoko, Utafiti na Huduma kwa Wateja wa Benki ya CRDB, Tully Ester Mwambapa akifafanua jambo kwa waandishi wa Habari kuhusu Benki hiyo kuanza mchakato wa kumtafuta mrithi wa nafasi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB.
Baadhi ya Wakurugenzi wa Benki ya CRDB wakimsikiliza Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dkt. Charles Kimei wakati atoa taarifa ya kuanza mchakato wa kumtafuta mrithi wa nafasi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Benki hiyo, unaotaraji kuanza mapema mwakani.
Sehemu ya wanahabari pamoja na wageni wengine.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad