HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Saturday, November 11, 2017

WIZARA YA AFYA YAWATAKA WANAWAKE KUPIMA AFYA ZAO ILI KUPAMBANA NA MAGONJWA YASIYOAMBUKIZI

Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.
Mkurugenzi wa kinga kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt Neema Rusibamayira amesema kuwa anafurahishwa na jitihada zinazofanywa  na taasisi zisizo za kiserikali kwa kuhakikisha wanapambana na magonjwa yasiyo ya kuambukiza.

Akizungumza kwa niaba ya Waziri wa Afya, Maendeleo ya jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Ummy mwalimu, Dkt Neema amesisitiza elimu juu ya masuala ya afya kwa akina mama kuweza kupata elimu zaidi kwani wao ndo waathirika wakuu wa ugonjwa wa kisukari.

Akitoa rai hiyo baada ya matembezi hayo yaliyoanzia Muhimbili mpaka viwanja vya Mnazi mmoja vikihusisha wadau mbalimbali, Dkt Neema amesema elimu juu ya masuala ya magonjwa yasiyoambukizi yatasaidia kupunguza kwa ongezeko la wagonjwa wa kisukari pia wananchi wawe na kawaida ya kupima afya zao mara kwa mara.

Matembezi hayo yameenda na kauli mbiu ya mwanamke na kisukari pia wadau walioweza kushirikiana kwa pamoja ni Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), TANCDA, LIONS Club na TDA ikiwa ni katika maadhimisho ya siku ya kisukari duniani yakienda na kauli mbiu ya mwanamke na kisukari.
 Mkurugenzi wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Benard Konga akizungumza baada ya matembezi ya hisani ya kuhamasisha wananchi kupambana na magonjwa yasiyo ya kuambukiza ikiwa ni katika maadhimisho ya siku ya kisukari duniani na mwaka huu yakienda na kauli mbiu ya Mwanamke na kisukari.

 Mkurugenzi wa kinga kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt Neema Rusibamayira akizungumza baada ya matembezi ya hisani ya kuhamasisha wananchi kupambana na magonjwa yasiyo ya kuambukiza ikiwa ni katika maadhimisho ya siku ya kisukari duniani na mwaka huu yakienda na kauli mbiu ya Mwanamke na kisukari.
 Wadau mbalimbali wakiwa katika matembezi ya hisani kuhamasisha wananchi kupambana na magonjwa yasiyo ya kuambukiza ikiwa ni katika maadhimisho ya siku ya kisukari duniani na mwaka huu yakienda na kauli mbiu ya Mwanamke na kisukari.
Mkurugenzi wa kinga kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt Neema Rusibamayira(wa kwanza kulia) akisalimiana na Mkurugenzi wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya, Benard Konga alipowasilia katika viwanja vya Mnazi baada ya matembezi ya hisani ya kuhamasisha wananchi kupambana na magonjwa yasiyo ya kuambukiza ikiwa ni katika maadhimisho ya siku ya kisukari duniani na mwaka huu yakienda na kauli mbiu ya Mwanamke na kisukari.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad