Mtendaji Mkuu Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) Bw. Godfrey Mngereza
(kushoto) akimuonyesha Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt.
Harrison Mwakyembe (mwenye kofia ya blue) eneo la jukwaa lilivyozingatia ubora wa
maonyesho alipofanya ziara katika taasisi hiyo kujua maendeleo ya ujenzi wa ukumbi
wa maonyesho wa BASATA jana Jijini Dar es Salaam.
Mkandarasi wa ujenzi wa ukumbi wa BASATA Bw. Novart Ludovick (wapili
kushoto) akimweleza Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt.
Harrison Mwakyembe (mwenye kofia ya blue) maendeleo ya ujenzi ulipofikia
alipofanya ziara katika taasisi hiyo kujua maendeleo ya ujenzi wa ukumbi wa
maonyesho wa BASATA jana Jijini Dar es Salaam.
Mtendaji Mkuu Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) Bw. Godfrey Mngereza
(katikati) akimuonyesha Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt.
Harrison Mwakyembe (kulia) picha inayoonyesha muonekano wa ukumbi wa BASATA
utakavyokua baada ya kumalizika alipofanya ziara katika taasisi hiyo kujua maendeleo
ya ujenzi wa ukumbi wa maonyesho wa BASATA jana Jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Maendeleo ya Sanaa Bibi. Leah Kihimbi (kulia) akizungumza baada
ya Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe
(kushoto) kukagua maendeleo ya ujenzi wa ukumbi wa BASATA jana Jijini Dar es
Salaam.
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe
(kulia) akizungumza na watumishi wa BASATA (hawapo pichani) baada ya kukagua
maendeleo ya ujenzi wa ukumbi wa BASATA jana Jijini Dar es Salaam. Kushoto ni
Mtendaji Mkuu BASATA Bw. Godfrey Mngereza.
Mtendaji Mkuu BASATA Bw. Godfrey Mngereza (kushoto) akimkabidhi zawadi ya
picha ya tingatinga Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison
Mwakyembe (katikati) baada ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa ukumbi wa BASATA
pamoja na kuzungumza na watumishi wa BASATA jana Jijini Dar es Salaam. Kulia ni
Mkurugenzi Maendeleo ya Sanaa Bibi. Leah Kihimbi.
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe
(wapili kushoto) akisikiliza wimbo uliotungwa na kuimbwa na mwanamuziki kutoka
Kongo unaosifia Uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt.
John Pombe Magufuli baada ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa ukumbi wa BASATA
pamoja na kuzungumza na watumishi wa BASATA jana Jijini Dar es Salaam. Kushoto ni
Mtendaji Mkuu BASATA Bw. Godfrey Mngereza.
Picha na Genofeva Matemu -WHUSM
No comments:
Post a Comment