HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, November 15, 2017

SPIKA NDUGAI APOKEA TAARIFA YA MKUTANO WA BUNGE LA AFRIKA ULIOFANYIKA KUANZIA TAREHE 6 MPAKA 20 OKTOBA, 2017 NCHINI AFRIKA YA KUSINI.

Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (kushoto) akimsikiliza Mjumbe wa Bunge la Afrika anaewakilisha Bunge la Tanzania, Mheshimiwa Stephen Masele (katikati) katika kikao kilichofanyika leo ofisini kwake Mjini Dodoma. wa pili kushoto ni Mwenyekiti wa Waheshimiwa Wabunge wa Bunge la Afrika wanaowakilisha Bunge la Tanzania, Mheshimiwa Asha Juma, wa pili kulia ni Mjumbe Mhe. David Silinde na kulia ni Katibu wa Spika, Ndg. Said Yakubu.
Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (kushoto) akimsikiliza Mwenyekiti wa Waheshimiwa Wabunge wa Bunge la Afrika wanaowakilisha Bunge la Tanzania, Mheshimiwa Asha Juma (kulia) katika kikao kilichofanyika leo ofisini kwake Mjini Dodoma.
 Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (kushoto) akizungumza na Waheshimiwa Wabunge wa Bunge la Afrika wanaowakilisha Bunge la Tanzania katika kikao kilichofanyika leo ofisini kwake Mjini Dodoma. wa pili kushoto ni Mwenyekiti wa Wabunge wa Tanzania, Mhe. Asha Juma, wa pili kulia ni Mjumbe Mhe. Stephen Masele na kulia ni Mjumbe Mhe. David Silinde.
  Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (wa pili kushoto) akipokea taarifa ya Mkutano wa Bunge la Afrika uliofanyika kuanzia tarehe 6 mpaka 20 Oktoba, 2017 nchini Afrika ya kusini, wakiongozwa na Mwenyekiti wa Wabunge wa Bunge la Afrika wanaowakilisha Bunge la Tanzania, Mheshimiwa Asha Juma (wa pili kulia) katika kikao kilichofanyika leo ofisini kwake Mjini Dodoma. kushoto ni Mjumbe, Mhe. Stephen Masele na kulia ni Mjumbe, Mhe. David Silinde.
(PICHA NA OFISI YA BUNGE)

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad