HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, November 16, 2017

RC Wangabo azihimiza Halmashauri kuongeza mashine za mapato kuongeza ukusanyaji

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo amewasifu wananchi wa kata ya Mtowisa, Tarafa ya Mtowisa, Wilayani Sumbawanga kwa kuonyesha mshikamano katika ujenzi wa shule ya Sekondari Vuma pamoja na ujenzi unaonendelea wa kituo cha polisi kitakachohudumia tarafa ya mtowisa.

Tarafa hiyo yenye kata 4 ina shule moja ya kidato cha tano na sita jambo alilosifu Mh. Wangabo kuwa imetimiza ilani cha Chama Tawala kwa kuwa na Shule moja ya aina hiyo kwa kila tarafa.

Amesema kuwa ataendelea kusisitiza kauli ya serikali ya awamu ya tano ya kuwa maendeleo hayana vyama, hivyo alisisitiza wananchi hao kutobaguana kwa itikadi zao bali wahimizane katika kutatua changamoto na kuleta maendeleo katika tarafa yao.

“Mmenivuti mliponieleza kwamba mnashirikiana katika nyanja mbalimbali, kuna majengo yale ya shule mnashirikiana na jengo hili la polisi mnashirikiana ili kuhakikisha kwamba changamoto mbalimbali zilizopo ndani yenu mnazitatua, hili limenifurahisha na ningependa muendelee nalo, na umeoja na mshikamano uliopo muudumishe bila ya kujali vyama vyenu.” Alisifu.

Ameyasema hayo katika Mkutano wa hadhara katika Kijiji cha mtowisa, kata ya mtowisa Wilayani Sumbawanga katika ziara yake ya siku mbili katika Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga yenye lengo la kutembelea miradi mbalimbali na kujitambulisha kwa wananchi.

Kwa upande wake diwani wa Kata ya mtowisa Mh. Edgar Malini alisema kuwa wananchi wa mtowisa hawana tabu wa kutoa ushirikiano ili kujiletea maendeleo wenyewe isipokuwa wamekuwa na kilio cha muda mrefu kuhusu umeme na maji.
 Mkuu wa Wilaya ya Sumbawanga Dk. Khalfan Haule akitoa maelezo ya kumtambulisha Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo kwa wananchi wa kijiji cha Zimba kata ya Mtowisa, Wilayani Sumbawanga. wakati walipofika kwenye kijiji hicho kuona kiwanda cha kukamulia alizeti. 
 Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo (wa tatu kutoka kulia) akiuliza swali kwa mhandisi wa maji wa Wilaya Patrick Ndimbo (wa kwanza kushoto) wakati walipotembelea mradi wa maji wa kutumia umeme wa jua mji mdogo Laela Wilayani Sumbawanga wenye thamani ya Shilingi Bilioni 1.8. 
 Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo akishiriki kutumia ala ya kigoda kuchekecha juu ya mtungi na kuzalisha sauti inayowezesha kuleta mlio kwaajili ya kunogesha nyimbo, Ni ala ya asili inayotumiaka katika ngoma za kitamaduni za Kifipa muda mfupi kabla ya kufanya mkutano na wananchi wa mji mdogo wa Laela. 
 Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo akimsalimia mmoja wa kinamama wa kikundi cha ngoma Laela Odila Maufi wakati alipokuwa akiingia katika viwanja vya shule ya Msingi Laela kwaajili ya Mkutano wa hadhara kujitambulisha kwa wananchi na kuongea nao.  

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad