HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, November 13, 2017

MSANII WA FILAMU, ELIZABERT MICHAEL "LULU" AHUKUMIWA KWENDA JELA MIAKA MIWILI

 Muigizaji wa Filamu, Elizabeth Michael 'Lulu' akiwa ni mwenye huzuni sana wakati akiwa katika Mahakama Kuu Dar es salaam kabla ya kusomewa hukumu ya kutumikia kifungo cha miaka miwili jela. 

Na Karama Kenyunko
Leo Novemba 13, 2017 Mahakama Kuu ya Tanzania kanda ya Dar es Salaam, imemuhukumu msanii maarufu wa filamu nchini, Elizabeth Michael "Lulu" kutumikia kifungo cha miaka miwili gerezani baada ya kupatikana na hatia ya mauaji ya bila kukusudia ya msanii mwenzake marehemu Steven Kanumba

Hukumu hiyo imesomwa na Jaji Sam Rumanyika ambaye amesema, ameridhika na ushahidi wa mashahidi wanne wa upande wa mashtaka na wazee wa baraza waliotoa maoni yao kuwa kweli mshtakiwa Lulu aliuwa bila ya kukusudia.

Lulu ametiwa hatiani chini ya kifungu cha sheria Namba 195 cha cha mwenendo wa mashtaka ya jinai.




No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad