HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, November 29, 2017

Kampuni ya Chai Bora yainunua kampuni ya Dabaga

Katika kutekeleza sera ya uwekezaji nchini ili kuendana na kasi ya serikali ya kuwa na Tanzania ya Viwanda ifikapo mwaka 2025, kampuni ya Chai Bora imeinunua kampuni ya Dabaga iliyokuwa ikitamba na bidhaa za kuongeza ladha za vyakula kama vile Dabaga tomato sauce , Pilipili Mbuzi, Mango pickle na bidha nyinginezo.

Kampuni ya Chai Bora imekuwa ikifanya shughuli zake hapa nchini tangia mwaka 1990, Chai Bora inaogoza kama chata ya kuzalisha majani ya chai, Ikijikita zaidi katika uzalishaji wa bidhaa kama vile majani kama vile Black Tea, Green Tea pia Kahawa aina ya Café Bora. Kwa kuwa imeanza kazi tangia mwaka 1990 hadi sasa ni takribani miaka 27 inaashiria ukuaji katika sekta husika ya bidhaa za Chai . Katika hiyo miaka 27 Chai Bora imeinunua kampuni ya Dabaga, imeongeza uzalishaji wa bidhaa tofauti na imeboresha kiwanda cha Dabaga Iringa na teknolojia za kisasa.
Uwekezaji huo ambao umehusisha teknolojia za kisasa na mitambo ya kisasa zaidi ni wazi kuwa itaongeza ufanisi kwenye uzalishaji wa bidhaa husika na kusukuma ongezeko la ajira nchini. Kupitia uzalishaji huo kwa sasa kiwanda hicho kimetoa ajira ya moja kwa moja na ajira isiyokuwa ya moja kwa moja kwa wakazi wa kijiji cha Ikokoto cha wilayani Ilula, Iringa. Wakulima ambao wanaojihusisha na shughuli za malighafi za viwanda kama hicho hasa wakulima, wasambazaji wa bidhaa za kilimo pamoja na watoa huduma wengine kama vile kampuni za ulinzi, usafi na hata watoa huduma za vyakula nao watanufaika na uwekezaji huo.

Mkurugenzi wa Chaibora, Mr.Kapila Mr.Kapila Ariyatilakakaalisema wakulima watanufaika kwa kuuza mazao yao hasa nyanya kwa kuwa kwa sasa kiwanda hicho kinahitaji nyanya tani 300 hadi 400 kwa mwezi. "Hii inaashiria kuwa wakulima wa nyanya wa ndani na nje ya Iringa watanufaika na uwepo wa kiwanda hicho hasa kwa kuuza bidhaa zao humo" anasema Mr.Kapila Ariyatilaka. Anasema wasambazaji wanaojihusisha na bidhaa za kilimo nao wamepata mwanya wa kuuza bidhaa zao na hasa wanaweza kununua kwa wakulima na kisha kuuza kwenye kampuni hiyo na hivyo kuongeza wigo wa ajira.

Anaongeza kuwa watoa huduma za ulinzi kwa maana ya kampuni za ulinzi nao hawapo nyuma katika kunufaika na kiwanda cha Dabaga. Vijana wengi wamepata ajira kiwandani hapo huku wengine wakifanya kazi za uuzaji wa vyakula kwenye migahawa ya kiwandani hapo na wengine hufanya vibarua vya hapa na pale kiwandani. Sasa kwa kuwa wafanyakazi ambao wameajiriwa moja kwa moja kiwandani hapo ni 35 huku wale waliopo kwa ajira za muda ni 45 ni wazi kuwa wanaongeza mzunguko wa fedha kwenye maeneo ya jirani.

Lakini kwa ajira hii na nyinginezo zitokanazo kwa uwekezaji huo wa Chai Bora ni wazi kuwa familia za watanzania zitanufaika na uwekezaji huo kwa kuwa wafanyakazi hao ndio watakaopeleka huduma nyumbani. Pia imeongeza hali ya maisha kwa wakazi wa eneo kilichopo kiwanda kwa kuwa wameanza kupangisha nyumba zao za kuishi kwa wafanyakazi wa kiwanda hicho.

Mzunguko wa fedha umeanza kuonekana kwenye jamii zao kwa kuwa kwa sasa wafanyakazi wa kiwanda hicho wananunua bidhaa kutoka kwa wafanya biashara hapo Ikokoto. Hiyo imesaidia kupunguza hali ya vijana kukaa vijiweni bila ya kuwa na kazi muhimu na kwa sasa wanakuwa wakipata angalau kipato kwa kufanya kazi kwenye kiwanda hicho au kujihusisisha na fursa nyingine kama kuuza bidhaa maeneo ya jirani na kiwanda.

Lakini pia kuna asilimia kubwa ya mafunzo yanatolewa na wataalamu wa kiufundi kutokea nje ya nchi hasa kutokea nchini China ambapo wachina ndio wamehusika na ujenzi wa mitambo hiyo ya kisasa ya kuzalishia bidhaa. Akizungumzia kuhusiana na changamoto kwenye uwekezaji wa Chai bora kwenye kiwanda cha Dabaga , alisema serikali ingetakiwa kuwa na sera ya kusaidia uwekezaji kwenye kilimo ambao unafanywa na wawekezaji nchini.

Alisema,"Ingetakiwa kuwepo kwa msamaha wa kodi hata kwa miaka mitano kwa uwekezaji wa asili ya bidhaa za kilimo ili kuongeza hamasa kwenye fani hiyo na kusaidia kukuza kilimo hapa nchini". Alisema, kwa sasa kampuni hiyo inalenga kuwakilisha vema kwenye soko la Afrika Mashariki na Kati na kwa hiyo ni vema ikasaidiwa kuimarisha mazingira bora zaidi ya kibiashara. Alisema, washindani wakubwa wa soko lake ni Red gold, American Garden, Pep Tang na Canadian. Lakini alibainisha kuwa changamoto nyingine kubwa inayowakabili kwa sasa ni kukosekana kwa umeme wa uhakika katika eneo la uwekezaji.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad