HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, June 22, 2017

CRDB YAWAKARIBISHA WATEJA WAKE KATIKA MAONYESHO YA SABASABA

Mkurugenzi wa Masoko, Utafiti na Huduma kwa Wateja wa Benki ya CRDB, Tully Mwambapa akizungumza na waandhi wa habari (hawapo pichani) kuhusu ushiriki wa Benki hiyo katika maonyesho ya Biashara ya kimataifa ya Dar es Salaam maarufu kama “Maonyesho ya Sabasaba”, yanayotarajiwa kuanza Juni 28, 2017 mpaka Julai 08, 2017 katika viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere, Kurasini, Jijini Dar es Salaam.

Benki ya CRDB imeahidi kushiriki kikamilifu na tutatoa huduma zote za kibenki kupitia “mobile branch” ambalo ni tawi kamili linalotembea na lenye uwezo wa kutoa huduma zote za kibenki za kutoa, kupokea na kutuma fedha, kununua fedha za kigeni na kupokea hundi, Hivyo Benki hiyo inawakaribisha wateja wake wote kutembelea tawi hilo.Kushoto ni Meneja Uhusiano wa Benki ya CRDB, Godwin Semunyu .
Mkurugenzi wa Masoko, Utafiti na Huduma kwa Wateja wa Benki ya CRDB, Tully Mwambapa akizungumza.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad