HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, June 20, 2017

BANDA AMALIZANA NA SIMBA, KUMWAGA WINO MUDA WOWOTE

Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.

Beki wa timu ya Taifa na klabu ya Simba Abdi Hassan Banda ameweka wazi msimamo wake wa kuendelea kuitumikia timu yake hiyo kwa mkataba wa miaka wa miaka miwili ila amewataka kuweka kipengele cha kumuachia iwapo atapata timu nyingine nje.

Ameyasema hayo wakati wa mazoezi ya timu ya Taifa kwa ajili ya kujiandaa na michuano ya COASAFA inayotarajiwa kuanza Juni 25 nchini Afrika Kusini. Banda amekubali kusaini kandarasi na timu yake ya Simba huku akiwa amepatiwa dau la maana ambalo limeweza kumshawishi kuendelea kusalia kwa wana msimbazi hao.

Taifa Stars inayojiandaa na michuano ya COSAFA Castle nchini Afrika Kusini baadaye mwezi huu, Banda amesema kwamba wakati wowote, Meneja wake Abdul Bosnia atafika Dar es Salaam ili wasaini mkataba huo mpya na Simba.
“ Mkataba wangu na klabu ya Simba umesalia siku tano, lakini tumeshafikia makubaliano na nitaendelea nao baada ya kusaini mkataba huo inaweza kuwa  kabla sijaenda Afrika Kusini au baada ya kurejea kutoka huko,"amesema Banda.

Ameweka wazi kuwa,  mazungumzo baina yake na uongozi wa Simba umekuwa mzuri na wenyewe wanajua makubaliano yao ili aweze kuongeza mkataba na kuendelea kuitumikia klabu hiyo na zaidi anamsubiri meneja wake aje kumalizana nao.

Banda yumo kwenye kikosi cha Taifa Stars, kinachotarajiwa kushiriki michuano ya Kombe la Mataifa ya Kusini mwa Afrika (COSAFA) Castle nchini Afrika Kusini kuanzia Juni 25, mwaka huu.

Taifa Stars iliyoweka kambi hoteli ya Urban Rose iliyopo iliyopo eneo la Kisutu, huku ikifanya mazoei Uwanja wa JMK Youth Centre, inatarajiwa kuondoka nchini Juni 22 kwenda Afrika Kusini kushiriki michuano ya COSAFA kama wa waalikwa kwa mwaka wa pili mfululizo na mara ya tatu kwa ujumla kihistoria.

Tanzania imepangwa kundi A pamoja na Mauritius, Malawi na Angola wakati Kundi B lina timu za Msumbiji, Shelisheli, Madagascar na Zimbabwe – na Botswana, Zambia, Namibia, Lesotho na Swaziland na wenyeji, Afrika Kusini zitacheza mechi maalumu za mchujo kuwania kuingia robo faina

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad