HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, March 2, 2017

MAHAKAMA YAIONYA NHC

Na Humphrey Shao, Globu ya jamii
Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam imelitaka shirika la Nyumba nchini (NHC) kuheshimu amri ya mahakama na kuondoa notisi walizowapa wakazi wa Keko mpaka kesi ya msingi itakapoisha.

Jaji Beatrice Mutungi wa mahakama hiyo amewaonya NHC leo baada ya wakili wa wapangaji wa magorofa ya Keko yaliyopo barabara ya uwanja wa taifa jijini, Daniel Lisanga kuwasilisha maombi ya kupinga wateja wake kuhamishwa.

Katika maombi hayo, Wakili Lisanga anapinga kitendo cha NHC kupeleka notisi ya siku 14 kwa wateja wake akitaka wahame katika nyumba hizo kabla kesi ya msingi waliyofungua haijaisha.

Akiongea mahakamani hapo, wakili Lisanga amesema kuwa Februari 27, mwaka huu wakati shauri hilo la ardhi lenye namba 23 likiendelea kusikilizwa, kwa makusudi  na huku wakijua kufanya hivyo ni kinyume cha sheria NHC Ilipeleka notisi ya siku 14 kwa wapangaji hao ikiwataka wahame.

Hata hivyo, NHC wameidharau amri ya mahakama iliyotolewa na Jaji Augustine Shangwa, Oktoba 6, mwaka juzi iliyowataka kutowabugudhi wapangaji hao mpaka kesi ya msingi itakapoisha.

NHC wanadaiwa kuwatumia Ubapa Auction Mart kwenda kuwaondoa wapangaji hao ambao ni jumla ya familia 60 zinazoishi katika block C,F,G na H.

Akizungumza nje ya mahakama wakili Lisanga amesema kuwa madai ya msingi ya shauri hilo bado yako mahakamani hivyo wamesikitishwa sana na kitendo cha kudhalilishwa kwa wateja wake kinachoendeshwa na NHC.

“Idara ya mahakama ni muhimili na inastahili kuheshimiwa na mtu yoyote ambaye yupo chini ya sheria”, amesema.

Hata hivyo mahakama haikuweza kuendelea na shauri hilo leo baada ya wakili wa NHC, Aloyce Sekule kushindwa kufika mahakamani
 Wakili Daniel Lisanga, akizungumza na wapangaji wa Shirika la nyumba la Taifa (NHC), mara baad aya kutoka mahakama ku jijini Dar es Salaam
Wapangaji wa Shirika la nyumba la Taifa (NHC),wakitoka nje ya mahakama kuu Tanzania.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad