HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, March 20, 2017

AZAM YAONDOLEWA SHIRIKISHO, YALALAMIKIA FITINA SWAZILAND

Kiungo wa Azam Frank Domayo akiruka juu kuuchukua mpira mbele ya mabeki mawili wa timu ya Mbabane Swallows Jana kwenye mechi ya Kombe la Shrikisho Afrika.


KLABU Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati, Azam FC, imeshindwa kutinga kwenye raundi ya mwisho ya mtoano ya michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika baada ya kufungwa na Mbabane Swallows mabao 3-0 jana jioni katika mchezo wa marudiano uliofanyika Uwanja wa Taifa wa Somhlolo, Swaziland.

Kwa ushindi huo wa Swallows, unaifanya kufuzu kwa raundi ijayo kwa jumla ya mabao 3-1 kufuatia ushindi wa bao 1-0 iliyoupata Azam FC katika mchezo wa kwanza uliofanyika Uwanja wa Azam Complex, jijini Dar es Salaam.

Kabla ya kuanza mchezo huo, wakati kikosi cha Azam FC kikiwasili uwanjani, mashabiki wa Mbabane kwa kushirikiana na polisi wa Swaziland walishirikiana kuifanyia vurugu timu hiyo kwa kuizuia isiteremke ndani ya basi.

Hali hiyo ilisababisha Ofisa Mtendaji Mkuu wa Azam FC, Saad Kawemba, kusukumwa, kupigwa na kuangushwa na polisi pamoja na mashabiki hao wakati akijaribu kupigania haki ya Azam FC kwa kushirikiana na maofisa usalama walioongozana na timu hiyo.

Maofisa usalama wa Azam FC waliokabiliana na mashabiki kuzima vurugu hizo waliongozwa na Kondo Idd almaarufu kama Karume, Juma Mdunguma, Kheri Mzozo, Edward Msimbe na Biggie Papa.

Katika hatua nyingine, Azam FC ililazimika kutoingia kwenye vyumba vya kubadilishia nguo baada ya kupuliziwa dawa kali, hali iliyoilazimu kubadilisha nguo kwenye basi za kuvaa katika njia ya kuingia vyumbani.

Mara baada ya mchezo huo, kikosi cha Azam FC kitaanza rasmu safari ya kurejea Tanzania kesho Jumatatu saa 6.15 kikiondoka katika Uwanja wa Ndege ya Kimataifa wa OR Tambo nchini Afrika Kusini kikipitia nchini Kenya kabla ya kutua jijini Dar es Salaam saa 3.00 usiku.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad