HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, February 7, 2017

WIZARA YA HABARI YAZINDUA PROGRAMU YA WADAU TUZUNGUMZE

Katibu Mkuu Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel akizungumza na waandishi wa habari (hawapo Pichani) leo Februari 07, 2017 Jijini Dar es Salaam kuhusu mkakati wa Wizara kuanza kuzungumza na wadau katika sekta zinazosimamiwa na Wizara yake.
Waandishi wa Habari wakifuatilia mkutano wa Katibu Mkuu Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel (hayupo pichani) akizungumza leo Februari 07,2017 Jijini Dar es Salaa kuhusu mkakati wa Wizara kuanza kuzungumza na wadau wa sekta zinazosimamiwa na Wizara yake. Picha na Raymond Mushumbusi

Na: Genofeva Matemu 
Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo imebuni na kutanganza Programu ya kushirikisha wadau inayoitwa wadau tuzungumze itakayosaidia wizara kupata vionjo, maoni, mawazo na fikra za wadau katika kuhakikisha kwamba Wizara inafanya kama wadau wake wanavyotegemea.

Hayo yamesemwa na Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel alipokua akizungumza na waandishi wa habari kutangaza programu hiyo yenye kauli mbiu ya kuitoa wizara ofisini kuipeleka kwa wadau leo Jijini Dar es Salaam.

Prof. Gabriel amesema kuwa Wizara imekua na kauli mbiu ya kuitoa Wizara Dar es Salaam kuipeleka mikoani na sasa inaendelea na mkakati wa kuitoa wizara ofisini na kuipeleka kwa wadau kwani Shabaa kubwa ya wizara ni kuhakikisha kwamba yale yanayofanywa na wizara jamii iyafahamu katika kutekeleza nia na hari ya hapa kazi tuu ya serikali ya awamu ya tano.

“Mpango wa programu ya wadau tuzungumze utafanyika kisekta ambapo utakua ni mkutano utakaoshirikisha mmoja wa viongozi wa wizara kukutanana na wadau na utakua na utaratibu madhubuti kwa kila mwezi siku ya jumanne saa nne asubuhi ambapo viongozi hao watakutana na vyombo vya habari wakiwa na wadau kujadili mambo ya kisekta” amesema Prof. Gabriel.

Mpango huu utahusisha Jumanne ya kwanza ya mwezi sekta ya habari na wadau wote wa habari, jumanne ya pili ya mwezi ni kwa ajili ya sekta ya Utamaduni na wadau wote wa utamaduni, jumanne ya tatu ya mwezi ni kwa ajili ya sekta ya sanaa na wadau wote wa sanaa na mwisho jumanne ya nne ya mwezi ni kwa ajili ya sekta ya maendeleo ya michezo na wadau wake.

Pamoja na mambo mengine program hii itatoa fursa kubwa sana kwa wadau kuleta mawazo yao ili wizara iweze kuwaingiza kwenye mnyororo wa thamani wa shughuli zake kwani wizara inatamani ifanye kwa mlengo ambao wadau weke wanatamani ifanyike.

Progamu hii itazinduliwa rasmi tarehe 14 Mwezi Februari mwaka 2017 hapa Jijini Dar es Salaam ambapo itahushisha sekta ya Utamaduni na hapo baadaye mikutano hii inaweza kufikiriwa na kufanywa kwa kanda. Mpango huu utahusisha pia Taasisi zilizo chini ya wizara.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad