HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, January 11, 2017

VODACOM TANZANIA FOUNDATION YAWAKUMBUKA WATOTO WA SHULE MAALUMU MKOANI NJOMBE

 Mtoto mwenye ulemavu wa ngozi wa shule maalumu ya msingi ya Mundindi wilayani Ludewa Mkoani Njombe, Yohana Mwaifuge(katikati) akipokea moja ya msaada toka kwa Meneja wa Vodacom Tanzania wa Mkoa huo, Benedict Kitogwa aliyekabidhi msaada huo jana  kwa niaba ya Vodacom Tanzania Foundation.Msaada huo wenye thamani ya shilingi Milioni 15/- ni Vyakula,Sabuni, Magodoro pamoja na mablanketi.
 Meneja wa Vodacom Tanzania Mkoa wa Njombe, Benedict Kitogwa(kushoto) akimsalimia mtoto mwenye ulemavu wa macho wa shule maalumu ya Mundindi wilayani Ludewa Mkoani humo, Robert Lwaizala wakati alipotembelea shule hiyo jana  kukabidhi msaada wa vitu mbalimbali wenye thamani ya shilingi Milioni 15/- kwa niaba ya Vodacom Tanzania Foundation.
Baadhi ya watoto wanaosoma katika  shule maalumu ya Mundindi wilayani Ludewa Mkoani Njombe, wakila chakula cha mchana na Meneja wa Vodacom Tanzania wa mkoa huo, Benedict Kitogwa(katikati)baada ya kukabidhi msaada wa vitu mbalimbali jana kwa niaba ya Vodacom Tanzania Foundation wenye thamani ya shilingi Milioni 15/- kama vile Vyakula, Sabuni, Magodoro pamoja na mablanketi.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad