HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, December 2, 2016

VIJANA WAKUBALI MAENDELEO ENDELEVU, WAAHIDI KUYAPELEKA VIJIJINI

Wakati wanachuo wa Chuo Kikuu cha Teofilo Kisanji (TEKU) cha mjini Mbeya wakiahidi kupeleka vijijini kampeni ya malengo ya maendeleo endelevu (SDGs) Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez amesema kwamba utekelezaji wa malengo hayo uko mikononi mwa vijana zaidi. Alisema nchini Tanzania zaidi ya nusu ya watu wake ni vijana hivyo wakielewa malengo hayo itakuwa rahisi kushawishi wengine kuhuisha maendeleo hayo na shughuli zao za kila siku huku wakitunza mazingira. Alisema shauri kwanini malengo yamekuwa mengi wakati yale ya Milenia yalikuwa nane tu, Mratibu huyo alisema kwamba suala si uwingi wa malengo bali maana yake na haja ya utekelezaji. 
Mkuu wa Chuo Kikuu cha Teofilo Kisanji (TEKU) cha jijini Mbeya, Dr. Daniel Mosses akimkaribisha na Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez aliyemtembelea ofisini kwake mjini Mbeya.(Picha zote na Zainul Mzige wa Modewjiblog)

Alisema MDGs (Malengo ya Millennia) iliacha masuala kadhaa bila uelekeo ikiwamo suala la mazingira na mabadiliko ya tabia nchi na hivyo kuwapo kwake kunahakikisha uwapo wa maendeleo endelevu kwa kuwa kila kitu kinategemea sana mabadiliko ya tabia nchi kwa sasa. Alisema ni matumaini yake kwamba kuzinduka kwa jamii ya vijana itasaidia kukabiliana na changamoto hizo za sasa za dunia. Kauli ya mratibu huyo iliungwa mkono na wanachuo hao ambao walisema kwamba wanaona uhalisia wa mahitajhi ya sasa na kwamba watawasilisha kampeni hiyo maeneo wanayotoka ili kuwapo na mabadiliko.
Mkuu wa Chuo Kikuu cha Teofilo Kisanji (TEKU) cha jijini Mbeya, Dr. Daniel Mosses akiwa kwenye mazungumzo na Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez aliyeambatana na Mtaalam wa Mawasiliano wa Shirika la Umoja wa Mataifa nchini, Hoyce Temu.

Kwa kuwa wengi ni vijana na kwa kuwa asilimia 75 ya vijana wanaishi vijijini, itakuwa heri kama walivyofundishwa na Umoja wa Mataifa kupeleka salamu vijijini ili kukabiliana na tatizo la mazingira na mabadiliko ya tabia nchi ambayo yanafumua misimu ya kilimo na upatikanaji wa mvua. Kushirikisha vijana ni suala la msingi sana, hasa ikizingatiwa kwamba sehemu kubwa ya vijana wanatoka vijijini ambako malengo ya maendeleo endelevu yana maana zaidi kwa umma, alisema Kidai Kabula Shaban, Mwanafunzi anayesomea Shahada ya Sanaa, Sosholojia na Kazi za Jamii.
Mkuu wa Chuo Kikuu cha Teofilo Kisanji (TEKU) cha jijini Mbeya, Dr. Daniel Mosses akizungumza machache kabla ya kumkaribisha Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez kuendesha semina ya malengo ya dunia (Global Goals) kwa wanafunzi wa chuo hicho iliyofadhiliwa na Umoja wa Ulaya (EU).

Amesema amefurahishwa mno na mpango huo wa kuelimisha vijana hasa utunzaji wa mazingira ili kukabiliana na tabia nchi. Alisema yeye alivyoelimishwa basi atahakikisha anawaelimisha wengine kuwa watekelezaji wa maendeleo hayo. Akirejea mazungumzo ya mwanafunzi huyo kwa niaba ya wenzake. Alvaro alisema amefurahishwa na mwamko wa vijana wa kutaka kujua malengo hayo na ni imani yake kwamba kwa kuwakujua wao basi jamii itaerevuka mapema zaidi.
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez akiendesha semina kuhusu malengo ya maendeleo endelevu (SDGs) kwa wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Teofilo Kisanji (TEKU) cha jijini Mbeya iliyofadhiliwa na Umoja wa Ulaya (EU).
Mtaalam wa Mawasiliano wa Shirika la Umoja wa Mataifa nchini, Hoyce Temu akiwapiga msasa wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Teofilo Kisanji jijini Mbeya wakati wa semina kuhusu malengo ya maendeleo endelevu (SDGs) iliyofadhiliwa na Umoja wa Ulaya (EU).
Mtaalam wa Mawasiliano wa Shirika la Umoja wa Mataifa nchini, Hoyce Temu akifafanua jambo wakati wa semina ya malengo ya maendeleo endelevu (SDGs) kwa Chuo Kikuu cha Teofilo Kisanji jijini Mbeya iliyofadhiliwa na Umoja wa Ulaya (EU).
Mwalimu wa Chuo Kikuu cha Teofilo Kisanji cha jijini Mbeya, Furaha Komoro akiuliza swali kuhusu juhudi za Umoja wa Mataifa katika kuhakikisha usawa wa kijinsia unakuwa na uwiano sawa pande zote.
Mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Teofilo Kisanji akishiriki kutoa maoni kwenye semina ya malengo ya dunia iliyoandaliwa na Umoja wa Mataifa na kufadhiliwa na Umoja wa Ulaya (EU).
Mwanafunzi anayesomea Shahada ya Sanaa, Sosholojia na Kazi za Jamii chuoni hapo, Kidai Kabula Shaban akiuliza swali kwa mkufunzi (hayupo pichani) wa malengo ya maendeleo endelevu (SDGs).
Pichani juu na chini ni sehemu ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Teofilo Kisanji jijini Mbeya walioshiriki semina ya malengo ya maendeleo endelevu (SDGs) iliyofadhiliwa na Umoja wa Ulaya (EU).



Mmoja wa washiriki akipitia kijarida cha malengo ya maendeleo endelevu (SDGs) katika semina iliyofanyika Chuo Kikuu cha Teofilo Kisanji jijini Mbeya.
Picha juu na chini ni Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez katika picha ya pamoja na wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Teofilo Kisanji cha jijini Mbeya waliohudhuria semina ya malengo ya dunia (Global Goals) iliyofadhiliwa na Umoja wa Ulaya (EU).
Pichani juu na chini ni semina maalum ya mabalozi wa malengo ya maendeleo endelevu (SDGs Champions/Global Goals Champions) wakipigwa msasa wa SDGs na Mtaalam wa Mawasiliano wa Shirika la Umoja wa Mataifa nchini, Hoyce Temu (hayupo pichani).
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez akikabidhi cheti kwa Balozi wa Malengo ya Maendeleo Endelevu (Global Goals Champion) Manafunzi wa Chuo Kikuu cha Teofilo Kisanji (TEKU) ambaye pia ni mrembo wa taji la Miss Mbeya 2016, Eunice Robert.
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez katika picha ya pamoja na mabalozi wa malengo ya maendeleo endelevu (SDGs) Global Goals Champions wakiwa wameshikilia vyeti vyao mara baada ya kuhitimisha semina maalum kwa mabalozi hao.
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez katika picha ya pamoja na mabalozi wa malengo ya maendeleo endelevu (SDGs) Global Goals Champions wa Chuo Kikuu cha Teofilo Kisanji (TEKU) cha jijini Mbeya wakiwa wameshikilia baadhi ya SDGs.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad