HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, November 18, 2016

WAZIRI MWIGULU NCHEMBA AFANYA MAZUNGUMZO NA BALOZI WA UHOLANZI NA UMOJA WA FALME ZA KIARABU, JIJINI DAR ES SALAAM

 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba akimfafanulia jambo Balozi wa Uholanzi nchini, Jaap Frederiks (katikati) wakati Balozi huyo alipomtembelea ofisini kwake, jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kujadiliana masuala mbalimbali ya ushirikiano kati ya Tanzania na Uholanzi. Kulia ni Eugene Gies ambaye ni Katibu wa Uchumi na Sera za Biashara wa Ubalozi huo nchini. Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba (katikati) akimsikiliza Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Balozi Simba Yahya alipokuwa anamfafanulia jambo Balozi wa Umoja wa Falme za Kiarabu, Abdulla Ibrahim Alsuwaidi (kulia) alipomtembelea Waziri Mwigulu ofisini kwake, jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kujadiliana masuala mbalimbali ya ushirikiano kati ya nchi hizo mbili. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba (katikati) akimsikiliza Balozi wa Uholanzi nchini, Jaap Frederiks alipokuwa anamfafanulia jambo Waziri huyo ofisini kwake jijini Dar es Salaam leo, walipokuwa wanajadiliana masuala mbalimbali ua ushirikiano kati ya Tanzania na Uholanzi. Kushoto ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Balozi Simba Yahya. Kulia ni Katibu wa Uchumi na Sera za Biashara wa Ubalozi huo nchini, Eugene Gies.  Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba (kushoto)akimsindikiza Balozi wa Umoja wa Falme za Kiarabu, Abdulla Ibrahim Alsuwaidi mara baada ya kumaliza mazungumzo yao yaliyofanyika katika ofisi ya Waziri Mwigulu, jijini Dar es Salaam leo. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba (kulia) akimkaribisha ofisini kwake Balozi wa Uholanzi nchini, Jaap Frederiks kwa ajili ya kufanya mazungumzo naye kuhusu masuala mbalimbali ya ushirikiano kati ya Uholanzi na Tanzania. Mazungumzo hayo yalifanyika katika ofisi ya Waziri huyo, jijini Dar es Salaam leo. Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad