HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, October 26, 2016

TANZANIA YAADHIMISHA SIKU YA MTOTO MWENYE KICHWA KIKUBWA NA MGONGO WAZI MOI MUHIMBILI JIJINI DAR

Mmoja wa Watoto wa wenye Kichwa kikubwa akiwa amebebwa na mzazi wake wakati wa maadhimisho ya siku ya Mtoto mwenye Kichwa Kikubwa na Mgongo wazi, yaliyofanyika kwenye Hospitali ya Muhimbili kitengo cha MOI, Jijini Dar es salaam.
 
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Hospitali ya Moi, Dk. Othmani Kiloloma akifungua rasmi sherehe za kuadhimisha siku ya mtoto wa kichwa kikubwa na Mgongo wazi Duniani,ambapo alisema wanakazi kubwa ya kutoa matibabu kwa watoto wenye matatizo ya mtindio wa ubongo na mifupa na mpaka sasa watoto takribani 202 wameshafanyiwa upasuaji na zoezi linaendelea Nchi nzima.
Mwenyekiti wa chama cha wazazi wenye watoto wenye vichwa vikubwa na mgongo wazi Bw. Hakim ambaye nae mtoto wake anamatatizo kama hayo akielezea kuwa kuna umuhimu wa kutoa elimu kwa kuwa watu wengi wanahusisha tatizo hilo na imani potofu, aliongeza kuwa watoto waliofanyiwa upasuaji mkoa wa Mbeya ni 18, Morogoro 12, Mwanza 50, na Izazi 14. na wamefanikiwa kuokoa Maisha ya watoto 185 katika mikoa 16 Tanzania.

Mmoja wa wazazi akiwa na Mwanae mwenye tatizo la Kichwa kikubwa.

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Hospitali ya Moi, Dk. Othmani Kiloloma (Kushoto) akipokea Msaada kutoka Duka la madawa la Nakiete.
 
Madam Sophia Mbeyela (Kulia) akitoa msaada kwa watoto hao.




Baadhi ya wazazi wakiwa na watoto wao wenye vichwa vikubwa.

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Hospitali ya Moi, Dk. Othmani Kiloloma wapili kutoka kushoto akipokea Msaada viti 15 vya kutembelea 'wheel chair' watoto kutoka kwa Mohamed Punjan Foundation.

Baadhi ya wauguzi wakiwa katika maadhimisho hayo




Baadhi ya wazazi na walezi na wazazi wenye kichwa kikubwa na Mgongo wazi wakiwa katika maadhimisho hayo.

Picha zote na Fredy Njeje

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad