HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, September 5, 2016

Wazazi Wajitokeza kwa Wingi kupima Watoto Wenye Matatizo ya Moyo

Baadhi ya wazazi na walezi wakisubiri kuingia kwenye chumba cha daktari kwa ajili ya watoto kuchunguzwa kama wana matatizo ya moyo. Watoto watakaobainika watafanyiwa upasuaji na wazazi watatakiwa kuchangia gharama. 
Na John Stephen, MNH

Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) leo imeanza kupima watoto bure ili kubaini kama wana matatizo ya moyo watachangia gharama za upasuaji. 

Wazazi na walezi wenye matatizo ya moyo wamejitokeza kwa wingi leo katika taasisi hiyo wakiwa na watoto na kupatiwa vipimo ili kubaini matibabu. 

Mkurugenzi Mtendaji wa taasisi hiyo, Profesa Mohamed Janabi amesema kwamba watoto watakaobainika kuwa na matatizo ya moyo watafanyiwa upasuaji.

“Watoto watakaobainika kuwa tatizo tutawafanyia upasuji, wazazi wanatakiwa kuchangia kiasi cha fedha ili kukamilisha matibabu kwa watoto husika,”amesema Profesa Janabi.

Taasisi hiyo imeanza shughuli ya kuwapima watoto ili kubaini kama wana matatizo ya moyo na kuwafanyia upasuaji. Pia, watu wazazi wametakiwa kujtokeza kwa ajili ya watoto kufanyiwa upasuaji.
Baadhi ya wazazi wakiwa na watoto katika chumba cha Dk Stella Mongella wakisubiri watoto wao kufanyiwa vipimo Leo kwenye Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI).
Leo Dk Sulenge Kubhoja wa taasisi hiyo, akimchunguza mtoto Lisa Mashauri (2), mkazi wa Kinyerezi jijini Dar es Salaam.
Dk Sulenge Kubhoja akiendelea na uchunguzi kwa mtoto Hellen Emmanuel kutoka mkoani Iringa.
Baadhi ya wazazi na walezi wakiwa na watoto wao leo nje ya taasisi hiyo kabla ya kuingia katika chumba cha daktari leo.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad